(i) Kuna ndoto ambazo zimebeba vitu vinavyohitaji tafsiri ili uweze kupata ujumbe uliomo ndani yake. Mfano wa ndoto kama hizi tunaupata katika Mwanzo 40:5 – 23
(ii) Kuna ndoto ambazo zimebeba vitu ambavyo maana yake iko wazi, na kwa ajili hiyo havihitaji tafsiri yake, ili kuupata ujumbe uliomo ndani yake. Soma mfano wake katika Mathayo 1:18 – 24.
(iii) Kuna ndoto ambazo zina ujumbe peke yake, bila kubeba vitu vyovyote zaidi ndani yake. Soma mfano wake katika Mathayo 2:12,22 na Mwanzo 31:24,29.
(iv) Mfasiri sahihi wa ndoto na ujumbe uliomo ndani yake ni Mungu tunayemwabudu katika Kristo Yesu; bila kujali chanzo cha ndoto uliyoota!
(i) Maandalizi yanahitajika kwa ajili ya hatua iliyo mbele yako, au hatua unayotaka Mungu akupe unapoomba katika maombi yako.
(ii) Kuota “shule” au “chuo” maana yake maandalizi ya hatua fulani iliyo mbele yako yanahitaji utaratibu maalumu.
(iii) Kuota “shule” au “chuo” ulichowahi kusoma zamani, ina maana kwamba kuna jambo lililotokea hapo ulilotakiwa “kuvuka” – lakini hukuweza kuvuka, na kwa hiyo kuna eneo limekwama kwenye maisha yako.
(iv) Watu mlio nao darasani katika ndoto ina maana watu mlio ngazi moja ya kimaandalizi(v) Kuota ndoto uko darasani na watu uliowahi kusoma nao zamani au unaota unarudia darasa, au unarudia mtihani – ina maana umekwama mahali kimaisha na unahitaji maandalizi ili kuvuka hapo.
(vi) Ukiota hukai darasani wakati wengine wako darasani; au hukai kwenye mtihani wakati wengine wanafanya mitihani – ina maana huna utulivu unaotakiwa uwe nao ili uweze kujiandaa vyema kwa hatua iliyo mbele yako.
(vii) Ukiota unafanya mtihani – ujue: au unapita mahali kimaisha ambapo unapimwa kiwango chako ulichofikia kimaandalizi; au mbele yako kuna kuja kipimo kwa ajili ya kujua ikiwa umefikia kiwango kinachotakiwa kwa wewe kuingizwa hatua nyingine ya maisha
(viii) Ukiota unaota unasoma, na ukaona na somo unalosoma, au ukaota unafanya mtihani na ukaona somo la mtihani huo – ina maana unaonyeshwa aina ya, au eneo la – maandalizi unalotakiwa kulifuatilia kimaandalizi
Kumbuka – huu ni mfano tu wa kutafsiri ndoto na kupata ujumbe uliomo ndani yake kwa kutumia neno la biblia.
No comments:
Post a Comment