MATUNDA UNAYOPASWA KULA NA VITU USIVYOPASWA KUFANYA WAKATI WA HEDHI - MRS. BENSON

Post Top Ad

Friday, 1 September 2017

demo-image



UNAWEZA KUPATA STORI ZETU MOJA KWA MOJA KWA KUBONYEZA 'LIKE' HAPA
rlx pb%2BApp
PUSH%2BBN%2B728%2BV1

KILIHOST%2BADS
« Piga 0652262137 kuweka tangazo lako hapa - Push kwa Buku tu »

MATUNDA UNAYOPASWA KULA NA VITU USIVYOPASWA KUFANYA WAKATI WA HEDHI

BewisaTV+Banner
hedhi
Mzunguko wa hedhi ni mzungu­ko wa kila mwezi am­bao mwanamke hu­upata, hali ambayo huleta kuto­kwa na damu kutokana na mimba kuto­tungwa.

Kwa hali ya kawaida hedhi ya kwanza hutokea katika umri wa miaka 12 -13 na kuendelea na hutokea pale ambapo tishu za ukuta wa mji wa mimba zinapobomoka na kutoka kama damu ukeni.

Tumbo la hedhi au mau­mivu wakati wa hedhi (pe­riod pains) au ki taalamu dismen­orrhea, ni maumivu yanayo­jitokeza sehemu ya chini ya tumbo au kiunoni wakati mwanamke anapoanza kupata siku zake au kabla ya hapo.

Maumivu ya tumbo wakati wa hedhi huanza pale mayai yan­apotoka ka­tika mirija (fallopian tubes) na kuteremka chini ya mirija hiyo wakati wa Ovulation.

Maumivu ya tumbo la he­dhi yapo ya aina mbili. Aina ya kwanza au (Primary Dysmenorrhea) ni maumi­vu yasiyokuwa na sababu zozote za kimsingi za kitiba. Katika aina hii maumivu ni ya kawaida na huhisiwa se­hemu ya chini ya tumbo na kiunoni

Aina ya pili au (Second­ary Dysmenorrhea) ni yale maumivu yanayojumuisha maumivu yanayosababish­wa na sababu nyinginezo za kitiba kama vile mata­tizo katika kizazi, ugonjwa wa nyonga (PID) na mata­tizo katika mirija ya mayai.

Magonjwa pia husaba­bisha mwanamke kusikia maumivu ya tumbo la he­dhi. Miongoni mwa ma­gonjwa hayo ni endome­triosis. Hii ni hali ambayo seli za ndani ya mfuko wa uzazi huanza kuoka nje ya fuko hilo, au hata sehemu nyinginezo.

Leo ninayo orodha ya matunda ambayo yakitumika huweza kupunguza ma umivu wakati wa kipindi hi­cho.
Matunda hayo ni:-

lov%252C+nanasi
NANASI
Hili ni miongoni kati ya matunda yenye uwezo wa kupunguza maumivu hayo yatokanayo na mzunguko wa hedhi, hii ni kutokana na tunda hili kuwa na viru­tubisho vyenye uwezo wa kuifanya misuli ya sehemu za siri za kike kuwa huru (kurelax) na hivyo kupun­guza uwezekano wa mau­mivu makali.

lov3
NDIZI
Kama utakuwa ni mfuatiliaji mzuri wa umuhimu wa matunda nadhani utakuwa umewahi kusikia kuhusu umuhimu wa ndizi hata kwa wanamichezo na im­ekuwa ikiwasaidia kureke­bisha misuli na kuondoa tatizo la kukaza kwa misuli mara baada ya mazoezi, hivyo basi tunda hili pia huweza kuwasaidia wa­nawake ambao wanapatwa na maumivu makali wakati wa hedhi na kupunguza au kuondoa hali hiyo kabisa.

Pamoja na kukueleza kuwa matunda hayo huweza kupun­guza maumivu wakati wa mzunguko la­kini ni vyema kuzingatia kuwa matunda hayo ya­napaswa kuliwa angalau siku mbili au moja kabla ya kuingia kwenye mzunguko wako ili kupata matokeo mazuri zaidi.

Pia unashauriwa kunywa tangawizi kila siku mara mbili, wiki moja kabla ya kupata mzunguko wako, pia maji ya kutosha kipindi cha mzunguko kwani nayo huwa na nafasi kubwa ya kusaidia kupunguza ki­wango cha maumivu hayo.

Papai bichi lililokomaa husaidia kupunguza mau­mivu ya hedhi unashau­riwa kulila mara kwa mara. Mboga za majani pia ni msaada mkubwa kwa ku­punguza maumivu.

Hiki ni kichocheo na  hutolewa kwenda kwenye ukuta wa kizazi kusaidia kushusha ukuta uliotengenezwa na kuandaliwa kwa kutungisha na kuimarisha mimba kumong’onyoa ukuta huo ili ukuta mwingine utengenezwe ili yaanze maandalizi mapya ya mzunguko unao fuata.

Inapotokea kuwa kiwango hiki cha Prostaglandini  kinakuwa kingi kupita kiasi kinasababisha kule kukuza  na kusinyaa kwa misuli ya mfuko wa kizazi kuwa kwa kiwango cha juu  na wenye kuambatana na maumivu makali sana isivyo kawaida.

JIHADHARI NA VYAKULA

Moja ya baadhi ya vitu vinavyo sababisha kiwango cha Prostaglandini kuwa juu kupita kiasi ni ulaji wa vyakula vinavyo sababisha mchakato mwilini mwako na kuvuruga utendaji kazi wa mwili wako na hatimaye kuvuruguka shughuli zingine.

Vyakula hivyo ni kama vile vyakula vyenye kiwango kikubwa cha ngano, kunywa vinywaji vyenye sukari nyingi na rangi kama juisi na soda ambavyo ni kemikali za viwandani. Matumizi ya pombe, kahawa, caffeine zote hivyo ni hatari sana kwa afya ya mwanamke wakati wa mzunguko wake wa hedhi.

Jiepushe kuwa na uzito kupita kiasi ndiyo maana asilimia kubwa ya wanawake wenye matatizo haya ya maumivu ya tumbo la hedhi huwa wana dalili zinazoambatana na matatizo mengine ya mfumo wa chakula kama choo kuwa ngumu, Hemmorhoids  (bawasili), tumbo kuuma/kujigawa na kadhalika.

Hivyo basi unatakiwa pia kuhakikisha huna mchakato wowote unaoendelea kwenye mfumo wa chakula ili uweze kutibu tatizo hilo. Hivyo ndivyo baadhi ya visababishi vya msingi vinavyosababisha Proglandini kuwa katika kiwango cha juu sana na kusababisha misuli ya mfuko wa kizazi kukaza kupita kiasi kwa kuambatana na maumivu makali hasa wakati wa hedhi.

Kuna wanawake wengine wanakuwa na matatizo ya kiafya katika mfumo wa uzazi ambayo sasa yanasababisha hedhi mbovu kwa mwanamke. Aina hii ya kisababishi huitwa kisababishi sekondari, jina hili linatokana na jinsi dalili za hedhi mbovu zinavyotokea baada ya mwanamke kuwa na matatizo ya kuwa hedhi mbovu kwa kuwa na sekondari ya ugonjwa katika mfumo wa uzazi. Magonjwa haya yanaweza kuwa kama Endometriosisi .

Huu ni ugonjwa ambao haujulikani kuwa unasababishwa na nini hadi sasa lakini hauwezi kuambukizwa hata kwa kutumia njia ya kujamiana, huu ugonjwa unasababishwa na zile seli za ukuta wa mfuko wa kizazi zinatoka zinaenda kujipandikiza popote nje ya mfuko wa kizazi na kuwa na sifa ile ile kama zinapokuwa ndani ya mfuko wa kizazi.

Mbali na endometriosisi pia hedhi mbovu kama dalili ya msingi inaweza kusababishwa na vimbe ambazo zinaota ndani ya mfuko wa kizazi, nje ya mfuko wa kizazi na kwenye misuli ya kizazi ambazo huita fibroids.

Wagonjwa wengi yenye fibroids hulalamika kupata hedhi mbovu.Wanawake wengine huchanyama maumivu wanayo pata wakati wa hedhi na maumivu ya maambukizi kwenye mirija ya uzazi yani PID (Pelvic Inflammatory Diseases) hii ni kwa sababu inaweza kuwa ulipata maambukizi kwenye via vya uzazi vya mwanzo halafu maambukizi hayo yakapanda hadi kwenye mirija ya uzazi na hatimaye kusababisha dalili hizo za kiuno kukaza na kuuma sana lakini ukitaka kutofautisha tatizo hilo zingatia kwamba maumivu yanayotokana na PID hayaambatani na siku za hedhi hivyo ndivyo unaweza kutofautisha kiurahisi kabisa.

Shaloom!

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *